SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: YANGA KUZISAKA POINTI TATU UGENINI.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Klabu ya Yanga ilifanya mazoezi yake ya mwisho jana jioni kwenye uwanja wa Essipong Sports mjini Sekondi, Ghana kwa ajili ya mchezo wao w...
Klabu ya Yanga ilifanya mazoezi yake ya mwisho jana jioni kwenye uwanja wa Essipong Sports mjini Sekondi, Ghana kwa ajili ya mchezo wao wa marudiano dhidi ya Medeama utakaochezwa leo Jumanne Julai 26.
Yanga ililazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Medeama kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa taifa takribani juma moja lililopita na kupata pointi ya kwanza katika mechi zake tatu ilizocheza.
Mabingwa hao wa Tanzania wanashika nafasi ya mwisho katika Kundi A hivyo watakuwa na kibarua kizito cha kutafuta ushindi ugenini katika mchezo wao wa nne katika hatua ya makundi.
Yanga iliondoka nchini siku ya Jumamosi Julai 23 kuelekea Ghana kupambana kuhakikisha inapata pointi tatu kwa mara ya kwanza tangu ilipofuzu kwenye hatua ya makundi kombe la shirikisho Afrika.


26 Jul 2016

About Author

Advertisement

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top