
BAADA ya Alphonce Simbu kufanya vyema kwenye
mashindano ya mbio za Mumbai Marathon, sasa chama cha riadha Tanzania, RT
chamkabidhi majukumu mengine.
Simbu ambaye kwenye
mbio hizo alifanikiwa kushika nafasi ya kwanza na kuondoka na medali pamoja na
kitita cha dola 67,000 ambazo ni sawa na Sh milioni 147 za Kitanzania, Agosti
mwaka huu anatarajiwa kushiriki mbio za World Athletic Championship zitakazofanyika
London, England.
Katibu Mkuu wa RT, Wilhelm Gidabuday, ameliambia Championi Jumatano kuwa: “Fedha alizopata zimegawanyika sehemu tatu na kufikia hizo dola 67,000, zawadi za mshindi wa kwanza ni dola 42,000, lakini kutokana na kufanya kwake vizuri kwenye Olimpiki alipata mwaliko maalum ambao ulikuwa na kipengele kwamba akishinda au akishindwa lazima apewe dola 15,000 na wastani mzuri wa kukimbia akapata bonasi ya dola 10,000.
“Kilichobaki sasa tunataka aende London kwenye mashindano ya
World Athletic Championship na kurudi na medali, tukipata medali huko ni
heshima kubwa kwani haya ni ya pili kwa ukubwa ukiondoa Olimpiki.”
Chanzo; Champion.
Post a Comment