SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: VAN GAAL AIBUKA NA KUKANUSHA TAARIFA ZA KUSTAAFU KWAKE.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
BAADA ya kukaa kimya kwa muda mrefu, aliyekuwa kocha wa zamani wa klabu ya Manchester United, Loius Van Gaal, ameibuka na kukanusha ...
Louis van Gaal


BAADA ya kukaa kimya kwa muda mrefu, aliyekuwa kocha wa zamani wa klabu ya Manchester United, Loius Van Gaal, ameibuka na kukanusha taarifa zilizokuwa zikisambaa ya kuwa amestaafu kufundhisha maswala ya soka.

Van Gaal amekuwa nje ya uwanja tangu atimuliwe na mabosi wa Manchester United mwezi May mwaka jana.

Jumatatu hii gazeti moja la Uholanzi De Telegraaf lililipoti ya kwamba Van Gaal amestaafu kufundisha soka sababu kubwa ikiwa ni kufiwa na mjukuu nwake.

Lakini akifanya mahojiano na kituo kimoja cha redio Cadena Ser, nchini Hispania, Van Gaal amesema japo mswala la kustaafu linawezakana, lakini bado halijafahamika.

Vilevile, Mholanzi huyo alitanabaisha kuikacha ofa ya klabu ya Valencia walipomtaka kuwa kocha wao mkuu.

“Kama nitaendelea au la, itategemea na ofa nitakazozipata” Alisema Van Gaal.
“Nimefundisha klabu nyingi hapa barani ulaya lakini nahisi nimekuwa sina maendeleo mazuri nikiwa kwenye ngazi ya vilabu”

“Siwezi kustaafu kwa muda huu, lakini nitaamua mwishoni mwa likizo yangu ambayo inaishia mwezi June au July”

Van Gaal ameshinda mataji 7 akiwa na vilabu mbalimbali kama vile AZ, Barcelona, Bayern n.k kabla hajaihamia Manchester United.





About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top