SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Claudio Ranieri: Tunafahamu Jinsi Ya Kuziba Pengo La Kante.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Mkufunzi wa mabingwa wa EPL, Claudio Ranieri amesema kuondoka kwa Kiungo wao Ngolo Kante hakuna haja ya kuthibitisha ya kuwa litakuwa...

Claudio Ranieri says Leicester remain ambitious

Mkufunzi wa mabingwa wa EPL, Claudio Ranieri amesema kuondoka kwa Kiungo wao Ngolo Kante hakuna haja ya kuthibitisha ya kuwa litakuwa pengo kubwa sana. Meneja wa Mbweha hao wa jangwani, amesema ana matumaini kutakuwa hakuna tena kupoteza kwa kuuza mchezaji na kuongeza ya kuwa hela zipo kwaajili ya kuboresha kikosi chao.

Kiungo mchezeshaji, raia wa Ufaransa, alikuwa anatumika katika kikosi hicho katika nafasi tofauti na kuisaidia Leicester kutwaa kombe la EPL msimu uliomalizika.

Kante 25 ameuzwa katika klabu ya Chelsea lakini mkufunzi wa klabu hiyo Ranieri amesema yuko bize kuhakikisha anafukia shimo lililoachwa na Kante aliyekuwa na umuhimu mkubwa klabuni hapo.

‘‘Nafikiri ni vilevile tu kama ilivyokuwa mwanzo tukiwa na Cambiasso” Alisema Ranieri. ‘‘Ilikuwa ni ngumu kupata mbadala wake, lakini tayari tumekwisha kamilisha, ni vilevile, tu, soccer linaendelea, hakuna kusimama”

N'Golo Kante has left Leicester to join Chelsea


‘‘Mpira unaweza ukanipotea mimi Wes [Nahodha wa mbweha], mtu yeyote lakini pia bado watu wakaendelea kucheza mpira huohuo, nafikiri tuna kikosi bora sana na subiri tuone, kama kuna kitu kingine cha ziada tutakuwa tunakihitaji, bosi wetu yupo tayari kununua”

Ranieri alikuwa akiyaongea haya kuelekea mchezo wao dhidi ya PSG katika kombe la ICC huko nchini China pamoja na Marekani na Austria. Na Leicester walikuwa wanapewa nguvu lakini pia Andy King kuweza kufuata nyayo za Jamy Vardy kwa kuweza kusaini mkataba mrefu kuwa klabuni hapo.

Ranieri believes Riyad Mahrez is happy to stay at Leicester


Ranieri pia amesema anatumai wachezaji wengine muhimu wa kikosi hicho kama vile golikipa Kasper Schmeichel pamoja na fowadi Riyad Mahrez wataendelea kuwepo kikosini hapo.

‘‘Klabu inafanya vizuri sana, nafikiri wanataka kubaki nasisi, kujaribu na kuboreka kila kukicha kama msimu uliopita ni vigumu sana, lakini tutakuwa bora” Alisema Ranieri.

‘‘Ni jambo la muhimu wamesaini na kubaki nasisi kuendeleza maisha ya Leicester wakiwa kama mabingwa na subiri tu tuone itakavyokuwa” Alimalizia Ranieri.



About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top