SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Klaus Allofs: Draxler anabaki Wolfsburg.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
. Mkurugenzi wa klabu ya FC Wolfsburg amesema mchezaji wao Julian Draxler ataendelea kubaki klabuni hapo kwa misimu mingine Zaidi mpa...


.

Mkurugenzi wa klabu ya FC Wolfsburg amesema mchezaji wao Julian Draxler ataendelea kubaki klabuni hapo kwa misimu mingine Zaidi mpaka hapo watakapoamua kumuuza klabu nyingine.
Klabu ya Asernal ya nchini England imekuwa inahusishwa juu ya kutaka kumsajili mchezaji huyo ambae alikuwa sehemu ya kikosi cha ujerumani kilichotolewa katika hatua ya nusu fainali ya mataifa ya ulaya, mashindano yaliyofanyika nchini ufaransa na timu ya taifa ya ureno kutawazwa mabingwa.
Lakini Allofs amesisitiza ya kuwa hawawezi kumuuza Draxler na kuweza kutanabaisha ya kuwa huenda aliyekuwa mchezaji wa klabu ya Chelsea Andre Schurrle akaihama klabu hiyo.
 ‘‘Kwa Julian Draxler, ni asilimia 100 ya kuwa hataondoka na hakutakuwa na mjadala Zaidi” Alieleza Allofs.
Wolfsburg wangependa kumwona Shurrle akiendelea kukua chini yao, lakini tetesi kutoka klabu ya Borussia Dotimund zimewafanya waweze kumwachia Shurrle afanye mazungumzo nao na endapo watakubaliana nae basi watamwachia aende zake.
Shurrle amemwambia mkufunzi wake ya kuwa Borussia Dotimund imemfanya aifikirie mara mbili na huenda akafanya maamuzi ya kuisaini klabu hiyo.
Draxler ana msimu mmoja klabuni Wolfsburg tangu ajiunge nao akitokea shakle wakati Shurrle alijiunga na klabu hiyo mwaka jana akitokea klabu ya Chelsea.



 

 



About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top