
NYOTA
wawili wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo na Gareth Bale watapambana na Antoine
Griezmann wa Atletico Madrid kuwania tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Ulaya.
Bodi
ya Soka Ulaya (UEFA) imetangaza orodha fupi ya mwisho ya wachezaji watatu wa
kuwania tuzo hiyo leo na wachezaji wa la Liga watupu watachuana, tena wote
kutoka timu za Jiji la Madrid.
Mshindi
wa tuzo hiyo atapatikana baada ya kupigiwa kura na matokeo yatatangazwa katika
Grimaldi Forum mjini Monaco Agousti 25.
Waandishi
wa Habari kutoka nchi zote wanachama 55 wa UEFA watawasilisha orodha yao fupi,
huku 54 wakipiga kura.
Post a Comment