SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: SIMBA YABANWA MBAVU MOROGORO.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Wekundu wa Msimbazi Simba SC baada mfululizo wa matokeo mazuri katika mechi zao za kirafiki, leo wakajikuta wakilala bao 1-0 kutoka kwa...

Wekundu wa Msimbazi Simba SC baada mfululizo wa matokeo mazuri katika mechi zao za kirafiki, leo wakajikuta wakilala bao 1-0 kutoka kwa timu ya Halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni KMC, mchezo ulifanyika mkoani Morogoro.
KMC walipata bao pekee katika mchezo wa jana kupitia kwa Rashidi Roshwa mnamo dakika ya 10 kufuatia kazi nzuri iliyofanywa na Emanuel Memba.
Simba, ambayo jana safu yake ya ushambuliaji ilikuwa ikiongozwa na Ame Ally ‘Zungu’ aliyetokea Azam kwa mkopo walikosa nafasi nyingi za wazi ambazo pengine zingeweza kubadili matokeo ya mchezo.
Simba wanatarajiwa kurejea jijini Dar es Salaam kati ya leo au kesho tayari kujiandaa na mchezo dhidi ya ya FC Leorpads ya Kenya kuelekea siku ya maadhimisho ya Simba day, ambapo kilele chake ni Agosti 8.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top