
Mchambuzi wa masuala ya soka mahiri
nchini Tanzania Dr. Leaky ametoa utabiri wake ya kuwa klabu ya Manchester City
ya nchini England ndiyo itakuwa bingwa wa msimu wa ligi kuu wa mwaka 2016-2017.
Dr Leaky ambaye tunatarajia kumwona
katika simu za karibuni kwenye kituo cha televisheni cha TV1, stesheni ambayo
imepewa majukumu ya kuonyesha ligi ya EPL msimu huu, ameyaongea hayo huku
akifafanua ya kuwa kwa sababu ya usajili mzuri alioufanya Pep Guardiola, basi
anafikiri kwamba Guardiola ndiye atakayeibuka kidedea wa mbio hizo
zinazotarajiwa kuanza rasmi tarehe 13 mwezi huu.
‘‘Katika miaka ya karibuni hakuna
amekuwa na kazi ngumu kama mtabiri wa hali ya hewa Kuna siku zilizopita hapa,
watabiri wa hali ya hewa wote waliomba kuacha kazi, kwa sababu walipokuwa
wakitabiri, yalikuwa yakifanyika vingine kama uligundua” Alisema Dr. Leaky.
‘‘Kila mara mambo yamekuwa yakienda
kinyume, anayeweza kutabiri sasa hivi mapema ligi ya Wingereza itakuwaje,
anataka kweli awe ni mtu mwenye roho ngumu, Lakini na mimi nina roho ngumu,
naweza nikakwambia mwaka huu bingwa nafikiri, atakuwa ni Pep Guardiola” Alisema
Dr. Leaky
Alipoulizwa na jopo la waaindishi wa
habari za kimichezo ni kwa nini ametupa karata yake kwa Guardiola, Dr. Leaky
alisema, ‘‘Kwa mfano sasa tuseme wale watu wanaobeti, unapobeti unaangalia nini,
unaangalia uwezo wa timu, unaangalia, huyu jamaa timu yake iko kiasi gani, ana
wachezaji wazuri kiasi gani, yeye mwenyewe ni mzuri kiasi gani, ameongeza
wachezaji wazuri kiasi gani. Kutoka katika kiwango alichokuwepo na hawa wa
akina Norito ambao amewaleta, watampeleka wapi? Namwangalia MAN U kutoka
alipokuwepo, na hata tukimleta Pogba na Ibrahimovic, na wote ambao amewaongeza,
je atakuwa amesogea upande gani, Unajua kwa bahati mbaya MANU alikuwa ni mtu
ambaye amekunywa sana, akawa anaelekea nyumbani, akawa anayumbayumba, watu
wakasema huyu ataanguka tu, lakini bado yeye akawa anawaambia aaah wapi sianguki
mimi naenda, badala ya kuanguka akafika akajigonga kwenye mti, akaanguka. Ndio
hayohayo, Man U ilikuwa kila mtu anamwona huyu ataanguka, lakini alikuwa
hajiamini anajipa matumaini, Sasa kutoka katika kile kiwango kufika mara moja
kuweza kuchukua ubingwa sio rahisi.”
Na Dr. Leaky akaendelea akisema mpinzani
pekee wa ManCity atakuwa ni Chelsea. Lakini alipoulizwa kwa upande wa Arsenal,
Dr. Leaky akasema mzee Wenger huu ndio mwaka wake wa mwisho.
‘‘Timu yangu sitaki kusema, lakini
kuna wengine ambao nafikiri utabiri wangu mwingine unataka, Mzee Arsene Wenger
ni mwisho msimu huu. Ama watamtoa watu kwa vile vigali vya Kariakoo vinavyobeba
mizigo, basi vile vya namna ile ndivyo vilivyombeba Van Gaal. Basi vile vya
namna ile vitambeba pia Wenger ama yeye atakataa kuifundisha timu yeye.”
Na Dr. Leaky akahitimisha akisema, ‘‘kwa
hiyo utabiri wangu, bingwa Guardiola, Mzee Wenger huu ndio msimu wake wa
mwisho.” Alimaliza Dr. Leaky.
Post a Comment