
Matatizo ya usafiri yameikumba timu ya
taifa ya kandanda ya Nigeria, Super Eagles.
Super Eagles wanatarajiwa kuwasili mjini Brazil saa 36 pekee
kabla ya kipenga cha kuanza kwa mashindano ya mwaka huu ya olimipiki ya Rio.
Wamiliki wa ndege walioikodisha walikataa kuendelea na safari
hadi nauli yote ya kikosi hicho itakapolipwa.
Kutokana na tofauti hiyo vijana wa Samson Siasia wanatarajiwa
kuwasili Brazil saa saba usiku wa kuamkia Ijumaa..
Yamkini kikosi hicho kilipofika Atlanta kilisusia kuendelea na
safari yao hadi shirikisho litakapowalipa pesa zilizosalia za nauli ya ndege.
Kampuni inayomiliki ndege hiyo ilidai kuwa pesa walizoahidiwa na
wizara ya michezo ya Nigeria haikuwa imefika katika akaunti zao kama
walivyoahidiwa.
Kundi B
§ Nigeria
§ Sweden
§ Colombia
§ Japan
Chelewa chelewa hiyo imeibua wasiwasi kwani Nigeria wanapaswa
kufungua dimba hilo dhidi ya Japan katika mji wa Manau siku ya Alhamisi.
Nigeria, iko katika kundi B pamoja na
Sweden, Colombia na Japan.
Nigeria ambao miaka 20 iliyopita iliweka rekodi ya kuwa
timu ya kwanza kutoka Afrika kutwaa nishani ya dhahabu inapigiwa upatu kufanya
vyema katika michuano huu.
Post a Comment