
Mchezo wa kirafiki kati ya mabingwa wa ligi kuu nchini Hispania
FC BARCELONA na mabingwa wa ligi kuu
nchini England, klabu ya Leicester city, the Fox, umemalizika kwa mabingwa wa
EPL kukubali kipigo cha magoli 4-2
Alikuwa ni Munir katika dakika ya 26 alipokwamisha mpira wavuni
na kuiandikia klabu ya Barca goli la kuongoza huku magoli mengine yakifungwa na
Suarez dakika ya 34, na Munir kurudi tena nyavuni dakika ya 45 na kufanya mpaka
mapumziko Leicester wakiwa nyuma kwa goli 3-0.

Kipindi cha pili kilianza kwa the fox kufanya mabadiliko na
kuwaingiza baadhi ya wachezaji wao wapya kama vile Ahmed Mussa, pamoja na Mendy
na dakika ya 48 Mussa akawanyanyua mashabiki wa Leicester kwa kuiandikia timu
yake goli la kwanza.
Wakati, mbweha hao wakihaha kutafuta magoli ya kusawazisha,
Mshambuliaji wao aliyesajiliwa toka CSKA MOSCOW ya Urusi akapachika bao la pili
dakika ya 67 na kurudisha nguvu ya kuweza kusawazisha magoli yote.
Rafael Mujica, ndiye aliyekata matumaini ya Mbweha hao baada ya
kuipatia timu yake goli la nne mnamo dakika ya 84 na mpaka mwamuzi anapuliza
filimbi ya mwisho, ubao ulikuwa unasomeka kama Barca 4-2 Leic.

Mchezo huo uliohudhuriwa na mashabiki takribani 42,879, ulikuwa ni
mchezo wa pili kwa Leicester kucheza na mabingwa wa ligi mbalimbali, wa kwanza
ukiwa ni dhidi ya timu ya PSG ambapo pia napo walikubali kipigo cha mbwa mwizi
cha magoli 4-0.

Baada ya mchezo huo, mkufunzi wa klabu ya Leicester, Claudio Ranieri
akasifu sana uwezo wa Mussa aliyemsajili toka CSKA Moscow na kusema atafanya
makubwa akiwa klabuni hapo.

‘‘Nimefurahishwa sana na Mchezaji Mussa, ni jambo la muhimu sana kwa
kikosi kama chetu kuwa na mchezaji mwenye maamuzi ya haraka sana na ameonyesha
uwezo wake” Alisema Ranieri.
Leicester city watakuwa na mechi wikiendi hii na klabu ya Manchester
United mechi ya ngao ya hisani kabla ya ligi kuu kuanza rasmi tarehe 13 ya
mwezi huu.
Post a Comment