SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Bastian Schweinsteiger Ajumuishwa Kwenye Kikosi cha wachezaji 25.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
KIUNGO mchezaji wa klabu ya Manchester United, Bastian Schweinsteiger amejumuishwa kwenye kikosi cha watu 25 cha timu hiyo. ...
Bastian Schweinsteiger in action for Manchester United



KIUNGO mchezaji wa klabu ya Manchester United, Bastian Schweinsteiger amejumuishwa kwenye kikosi cha watu 25 cha timu hiyo.

Schweinsteiger 32, bingwa wa kombe la dunia mwaka 2014  na timu ya taifa ya Ujerumani, alikuwa ameambiwa na kocha mkuu wa klabu hiyo kwamba hayupo tena kwenye mipango yake na hivyo atafute timu nyingine ya kwenda kuichezea.

Nahodha huyo wa timu ya taifa ya Ujerumani, alistaafu mapema mwa wiki iliyopita baada ya kuifungia timu yake ya taifa magoli 24 kati ya mechi 121 alizocheza nahodha huyo.

Klabu zote 20 za premia zinatakiwa kuwasilisha majina ya wachezaji 25 ambao kabla ya saa moja kwa majira ya saa za Africa Mashariki.

Wachezaji chipukizi kama vile Marcus Rashford, Luke Shaw na Anthony Martial wanaonekana  kupewa nafasi kwenye kikosi hicho cha mabingwa wa zamani wa EPL.

Schweinsteiger, aliyesajiliwa kwa kandarasi  ya miaka mitatu mwaka jana, alikuwa anafanya mazoezi peke yake na vijana wa miaka 23 tangu Mourinho amekuwa kocha wa klabu hiyo.

Nyota huyo wa zamani wa klabu ya Bayern Munich amesema yuko tayari kama timu itakuwa inamhitaji, wakati huo kocha Mourinho amesema Paul Pogba, Marouane Fellaini, Morgan Schneiderlin, Ander Herrera na Michael Carrick ndio wapo tayari kwenye kikosi chake

"Tuna wachezaji watano kwenye sehemu mbili” Mourinho alisema.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top