SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: TAIFA STARS TAYARI KWA KUIKABILI SUPER EAGLES.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
TIMU ya taifa ya Tanzania Taifa Stars, imewasili salama nchini Nigeria tayari kwa kuivaa timu ya taifa ya Nigeria katika mechi ya...




TIMU ya taifa ya Tanzania Taifa Stars, imewasili salama nchini Nigeria tayari kwa kuivaa timu ya taifa ya Nigeria katika mechi ya kufuzu kuwania tiketi ya kombe la mataifa ya Africa za mwakani, nchini Gabon.

Kundi la kwanza liliwasili Abuja jana kwa kutumia shirika la ndege la Ethiopia na kusafiri kwenda Uyo kwa kutumia jet.

Mwanasheria mkuu wa shirikisho la mpira nchini Nigeria, Tunde Aderibigbe aliupokea msafara huo na kusafiri nao mpaka Uyo kabla ya katibu wa NFF kuwapokea huko mji wa Uyo.

 


Taifa Stars walionekana wakiwa na amani huku wakiwa kwenye basi lao special walilokuwa wamekodiwa wakielekea kwenye hotel ya Meridian huku wakitarajiwa kufanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja watakaochezea hapo kesho.

Taifa Stars watakuwa wakisaka ushindi wao wa kwanza baada ya kucheza michezo mitano dhidi ya Nigeria wakiwa wameambulia patupu.

 


Katika michuano ya kufuzu kombe la dunia mwaka 1982, timu hizi zilitoka sare ya 1-1 mjini Lagos kabla ya Tanzania kukubali kichapo cha goli 2-0 hapa Dar es salaam, magoli yaliyofungwa na John Chidozie na Christian Nwokocha.

Super Eagles waliokuwa wamepangwa kucheza na Tanzania mwaka 1986, mwaka huu wamepangwa tena kundi moja huku mchezo wa kwanza ukimalizika jijini Dar es salaam kwa sare tasa,

Timu ya taifa ya Nigeria, imejipanga kuutumia mchezo huo kama ni mchezo wa kujiandaa na mechi ya awali ya kusaka tiketi ya kufuzu kombe la dunia la mwaka 2018 dhidi ya timu ya taifa ya Zambia.





About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top