SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: mazembe yatwaa pointi tatu ugenini.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
                          yanga yakubali kichapo picha na shaffih Na Charles Kunji. Hakika ngoma ya mwana haikeshi,  ...
                         yanga yakubali kichapo


IMG_0294
picha na shaffih



Na Charles Kunji.


Hakika ngoma ya mwana haikeshi,  na ushindi wa klabu ya yanga wa kwanza katika mashindano ya shirikisho barani afrika bado ni kitendawili.
Baada ya kupoteza mechi yao ya kwanza ugenini dhidi ya MO Bejaia ya Algeria, leo klabu ya yanga walikuwa nyumbani wakikipiga dhidi ya TP Mazembe mchezo uliomalizika kwa Yanga kupoteza tena kwa goli 1-0.
Goli la Mazembe lilitokana na mpira wa adhabu ndogo baada ya Kelvin Yondani kumuangusha Thomas Ulimwengu nje kidogo ya eneo la hatari. Mpira wa adhabu ndogo ulimfikia Merveille Bope na kuupachika kambani baada ya mabeki wa Yanga kushindwa kuuondosha kwenye eneo lao la hatari.
Tayari Yanga imeshacheza mechi mbili kwenye hatua ya makundi, wamefungwa zote kwa goli moja huku wao wakiwa bado hawajafunga bao hata moja katika mechi walizocheza.
Klabu ya yanga iliweza kuwatumia wachezaji wapy waliosajiliwa kama Juma Mahadhi aliyetoka timu ya coastal union iliyoshuka daraja na mahadhi kuonyesha mchezo wa kuvutia katika mechi yake ya kwanza ya kimataifa.
Katika kundi A, Tp mazembe wanaongoza kundi hilo wakiwa wamecheza mechi mbili na kujikusania pointi 6 huku wakiwa wamefunga magoli manne na kufungwa goli moja pekee goli lililofungwa kwenye ushindi wao wa goli 3-1 dhidi ya klabu ya kutoka nchimi Ghana Medeama FC.
Mchezo mwingine katika kundi hili utakuwa kesho wakati timu ya Medeama itakapokuwa nyumbani kuikaribi9sha klabu ya kutoka Algeria, timu ya Mo Bejaia.




About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top