SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Franz Backenbauer achunguzwa kwa kombe la dunia la 2006
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
VIONGOZI wa mashtaka nchini Uswizi wameanzisha uchunguzi wa uhalifu kuhusu mchezaji wa zamani nchini Ujerumani Franz Backenbauer ...
Franz Backenbauer



VIONGOZI wa mashtaka nchini Uswizi wameanzisha uchunguzi wa uhalifu kuhusu mchezaji wa zamani nchini Ujerumani Franz Backenbauer na wengine watatu kuhusu ombi la Ujerumani la kombe la dunia la mwaka 2006.

Kama wanachama wa kamati ya maandalizi ya kombe hilo, wanatuhumiwa kufanya udanganyifu, ulanguzi wa fedha na utumiaji mbaya wa fedha.

Baadhi ya uhalifu huo ulitekelezwa katika taifa la Uswizi.

Bwana Backenbauer ambaye aliongoza ombi hilo amekana kuhusika na ufisadi.
Mnamo mwezi Oktoba, alisema kuwa alifanya makosa katika shughuli yote ya ombi hilo mwaka 2000, lakini akakana kwamba kura zilinunuliwa.

Mnamo mwezi Machi, Shirikisho la soka duniani Fifa lilianza kuwachunguza watu sita kwa jukumu lao katika ushindi wa kuandaa haki za kombe hilo la dunia mwaka 2006.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top