Picha na salehe jembe. |
SAKATA la mwenyekiti wa klabu ya Yanga, limechukua sura mpya
leo baada ya wanachama wa klabu hiyo kukubaliana kwamba moja ya wazee wa klabu
hiyo, Mzee Akilimali, asimamishwe kwa muda, kwa
kile kinachodaiwa kwamba ni moja ya watu waliopelekea Manji aachie nafasi
hiyo ya uwenyekiti pamoja na kusitisha zoezi la kuikidosha klabu hiyo kwa miaka
kumi.
Hapo jana Yusuf Manji alitangaza nia yake ya kutaka kujiuzulu
kuwa mwenyekiti wa klabu hiyo ya jangwani na kusema kuwa kuna watu wanaofanya
yeye afikie maamuzi hayo kwani matusi yamezidi sana.
Aidha, baada ya wanachama kukutana leo makao makuu ya klabu
hiyo yaliyopo mtaa wa jangwani, wengi wao walikuwa wanataka mzee Akilimali
asimamishwe kwa muda kwani ndiye cha cha matatizo yote ya hapo klabuni.
Wakati alipopigiwa simu na mtandao wa www.salehejembe.blogspot.com,
mzee Akilimali alisema kuwa amekwenda kumaliza tofauti na hivyo wamsubiri
atarudi.
Hata hivyo, baada ya kuonekana kwenye makao makuu yay a klabu
hiyo, wanachama wengi wa klabu hiyo waliokuwa wanaongea kwa jazba, walitaka viongozi
wa klabu hiyo wamsimamishe mzee huyo kwa muda kwani amekuwa ni kikwazo klabuni
hapo.
Hata hivyo, kutokana na taarifa za ndani za www.charleskunji.blogspot.com,
imeripotiwa kwamba kikao cha viongozi wa klabu hiyo ya jangwani, wamekubaliana
kumsimamisha mzee Akilimali kwa muda, ili kupisha mambo mengine yaendelee ndani
ya klabu, kwani kwa uwepo wake, ni kama kikwazo kwa baadhi ya vitu kutokea.
Suala la Manji la kujiuzulu bado halijabatilishwa na
mwenyekiti huyo, na uongozi wa klabu ya Yanga, wanasubiri barua rasmi ya
kiongozi huyo kama kweli anataka kujiuzulu, ingawaje bado kuna taarifa ambazo
zimekuwa zikivumishwa ya kwamba Manji atarejea klabuni hapo.
Post a Comment