Pacquiao, 37, bingwa
wa zamani wa dunia, ametangaza kwamba atarejea licha yake kutangaza kwamba
angestaafu baada ya kumshinda Timothy Bradley mwezi Aprili.
Promota wake Bob Arum
alisema mwezi uliopita kwamba mwanabondia huyo kutoka Ufilipino angepigana tena
mwaka huu.
"Maisha ya
kustaafu hayamfai Manny kwa sasa," smeneja wa Pacquiao Michael Koncz
aliambia gazeti la Los Angeles Times.
"Ndondi zimo
kwenye damu yake."
Pacquiao na kundi lake
watakutana 10 Agosti mjini Manila kuamua iwapo pambano hilo dhidi ya Vargas,
27, litaandaliwa Los Angeles au Dubai.
Pacquiao alishinda
uchaguzi wa useneta Ufilipino mwezi Mei.
Vargas alitwaa ubingwa
mwezi Machi baada ya kushinda raia mwenzake Sadam Ali.
Post a Comment