SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: SIMBA YAREJEA DAR ES SALAAM.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Klabu ya wekundu wa msimbazi Simba imehamisha kambi yake toka mjini Morogoro hadi jijini Dar es salaam katika hoteli ya Dege Beach ...



Klabu ya wekundu wa msimbazi Simba imehamisha kambi yake toka mjini Morogoro hadi jijini Dar es salaam katika hoteli ya Dege Beach kwa ajili ya kuendelea kujiandaa na siku ya Simba day itakayofanyika siku ya jumatatu tarehe nane ya mwezi huu ambapo wataadhimisha miaka 80 ya klabu hiyo.

Wakiwa Morogoro, Klabu ya Simba ilifanikiwa kucheza mechi nne za kirafiki ambapo walifanikiwa kushinda mechi tatu na kupoteza mchezo wao wa mwisho dhidi ya klabu ya KMC.


Klabu hiyo iliyo chini ya mwlimu Joseph Omog, raia wa Cameroon itajitupa uwanjani kucheza dhidi ya klabu ya Leopords ya nchini Kenya mchezo ambao wangecheza na klabu ya Zimbabwe japo klabu hiyo ya Inyerclube ikajitoa mapema.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top