Mwana dada huyo amefikia hatua hiyo kwa ushindi wa 7-5
6-1 dhidi ya King.
Johanna Konta ambaye katika uchezaji Duniani yuko kwenye
nafasi ya 14, katika hatua inayofuata atakutana na Mmarekani Varvara Lepchenko
Wakati mashindano ya
Rogers Cup yakiendelea, idadi ya wachezaji wa tenesi kuendelea kujiengua katika
mashindano ya Olympic Yazidi kuongezeka baada ya mchezaji Belinda Bencic
anayeshikila namab 16 kwa viwango vya tenisi duniani kujitoa katika mashindano
ya Olympic yatakayoanza tarehe 5 ya mwezi ujao.

Bencic 19, raia wa Uswis
alilazimika kujitoa katika raund ya pili ya Wembleydon baada ya kupata maumivu
ya kifundo cha mkono, ametoa taarifa kupitia mitandao yake ya kijamii ya kuwa
hatoshiriki Olympic na badala yake muda wote huo atakuwa akijianda na
mashindano ya US Open ambayo yanatarajiwa kuanza tarehe 29 ya mwezi ujao, siku
moja baada ya Olympic kufikia kikomo chake.
Hivyo list ya wachezaji
wa tenisi ambao hawatoshiriki Olympic ni Maria Sharapova ambae yeye alifungiwa
kwa muda baada ya kukutwa na hatia ya kutumia dawa za kusisimua misuli, Lakini
pia Victoria Azarenka nae hatashiriki kwa sababu ya kuwa na ujauzito pamoja na
Simona Halep pamoja na Karolina Piscova.
Post a Comment