
Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp amesisitiza kwamba yeye si
muumini wa matumizi makubwa ya fedha linapokuja suala la usajili wa wachezaji
na kusema kwamba kutumia mil 100 kwa ajili ya kununua mchezaji ni njia sahihi
ya kuendesha soka.
Mjerumani huyo ameongeza
wachezaji Sadio Mane na Georginio Wijnaldum, lakini uhamisho wa wachezaji hao
hauwezi kufananisha na ule wa paundi mil 100 unaoripotiwa kufanywa na
Manchester United kwaajili ya kunasa saini ya Paul Pogba kutoka Juventus.
Hata hivyo, Klopp
amesema kwamba hana mpango wa kufanya usahihi wa aina hiyo, na kueleza wasiwasi
wake juu ya hasara inayoweza kupatikana kutokana na kiwango hicho cha fedha.
“Kama unanunua mchezaji
mmoja kwa paundi mil 100 na halafu anapata majeraha, hapo ndipo utakapoona
hasara yake.”
“Kikubwa ninachopenda
mimi ni kuhakikisha najenga timu imara yenye wachezaji wenye umoja na
kufanikiwa kwa pamoja.
“Timu nyingine zinaweza
kwenda kutafuta wachezaji wa gharama kubwa. Nataka niwe tofauti kidogo, lakini
pia ningefanya tofauti hata kama ningekuwa na kiasi hicho cha fedha.
“Sijui ni kiasi gani cha
fedha ambacho tungeweza kutumia kwasababu hakuna aliyeniambia, hapana huwezi
kufanya hivi’.
“Kama natumia pesa, ni
kwasababu najaribu kujenga timu, timu halisi. Barcelona walifanya hivyo.
Unaweza kushinda ubingwa, unaweza kushinda mataji, lakini kuna jinsi ambavyo
unahitaji kushinda.”
Klopp amesema kwamba
hana mpango wowote wa kushinda na vilabu vingine katika kuwania wachezaji.
Kocha huyo wa zamani wa
Borussia Dortmund amesema angependa zaidi kuangalia umuhimu wa mchezaji ambaye
anaweza kuwa na faida kwa timu yake.
Klopp amesema: “Kama
wote mnaogelea kwenye bwawa moja, basi lazima litakuwa dogo – na hatimaye
hamuwezi kutosha, sasa ndivyo ilivyo kwenye uwanaiaji wa wachezaji.
“Kuna wachezaji wengi tu
nje ya bwawa, wachezaji wazuri kwa hatima ya baadaye. Tunajitahidi kadri
tuwezavyo kuwapata.
“Mchezaji mzuri wa msimu
uliopita ni vizuri kumfahamu lakini inavutia zaidi kujaribu kutafuta mchezaji
ambaye siku za usoni anataraji kuwa mchezaji bora.
“Kama unaweza kufanya
hivyo sasa, unaweza kuwa usajili rahisi kuliko wote. Na hivyo ndivyo
tunavyojitahidi kufanya.
“Ni suala tu la kuwa
mbunifu, kwasababu ubunifu ni jambo zuri sana. Ni suala la kutafuta wachezaji
ambao wanaweza kwenda pamoja na sisi.”
Post a Comment