SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: SARE ZATAWALA AFCON
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
MASHINDANO ya AFCON yanayoendelea huko nchini Gabon, yamezidi kushika kasi baada ya kushuhudia leo mchezo mmoja ukipigwa. Baada y...
Riyad Mahrez is congratulated by Nabil Bentaleb


MASHINDANO ya AFCON yanayoendelea huko nchini Gabon, yamezidi kushika kasi baada ya kushuhudia leo mchezo mmoja ukipigwa.

Baada ya hapo jana kutawala kwa sare mbili zimwi hilo limeendeleea tena leo kwa mchezo wa awali ambapo Mbweha wa jangwani, timu ya taifa ya Algeria ililazimisha sare baada ya kutoka 2-2 dhidi ya timu ya taifa ya Zimbabwe.

Magoli ya Algeria yamefungwa na mshambuliaji wa klabu ya Leicester, Riyad Mahrez wakati magoli ya Zimbabwe yamewekwa kimiani na Kudakwashe Mahachi na Nyasha Mushekwi.

Kwa matokeo haya yanafanya mpaka sasa kutokuwepo kwa timu yeyote ambayo imeandikisha ushindi baada ya hapo jana wenyeji kubanwa mbavu na Guinea Bisau wakati Burki na Faso wakiwabana mbavu Cameroon.


 Mchezo unaotarajia kuanza hivi punde ni kati ya Senegal watakaowavaa Mali.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top