SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Kante kufanyiwa Vipimo Vya Afya hapo Kesho.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Klabu ya Chelsea imekubali kutoa kitita cha Pauni 32mil kwa ajili ya kupata kandarasi ya kiungo wa klabu ya Leicester City Ngolo Ka...

Claudio Ranieri (left) has previously said he wants Kante to stay at Leicester


Klabu ya Chelsea imekubali kutoa kitita cha Pauni 32mil kwa ajili ya kupata kandarasi ya kiungo wa klabu ya Leicester City Ngolo Kante. Taarifa na skysport.
Leicester City imlimpa Kante kandarasi ya miaka minne kabla ya mashinfano ya mataifa ya ulaya yaliyofanyika nchini Ufaransa, lakini raia huyo wa Ufaransa ameiambia klabu hiyo ya kuwa anataka kujiunga na klabuni ya Chelsea.
Knte 25, atakuwa na vipimo vya afya wikiendi hii kabla hajajiunga na klabu ya Chelsea huko Austria ambako ndio wameweka kambi wakijiandaa na msimu unaokuja ambapo ataweza kuzungumza hatma ya mkataba wake.
Mkufunzi wa klabu ya Leicester city Claudio Ranieri amesisitiza ya kuwa angependa kuona Kante akiendelea kuihudumu kabu hiyo,  lakini ameelewa ya kuwa Knte kumbe anataka kuondoka klabuni hapo. Alisema, ‘‘sihitaji kumpoteza Kante, sihitaji kabisa, lakini ningejua tu kama alikuwa anataka kuondoka”
Kante alikuwa na msimu bora kabisa akiwa na Leicester city na akiisaidia timu hiyo kutwaa ubingwa wa EPL kwa mara ya kwanza katika historia ya klabu hiyo huku akicheza mechi 37 pekee. Kane alijiunga na Mbweha wa jangwani akitokea klabu ya Caen inayoshiriki ligi ya Ufaransa Ligie 1 na kuitwa kwenye timu ya taifa ya ufaransa na kuweza kucheza chunu ya Deschamps.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top