
Timu ya taifa ya Ukraine imemwajili Andriy Shevchenko
kuwa kocha kuchukua nafasi ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo Mykhaylo Fomenko ambae amesitishiwa mkataba
wake wa miaka miaka minne.
Shevchenko 39, aliyewahi kuzichezea timu za Chelsea
pamoja na AC MILAN ya Italia, ameichezea timu ya taifa ya Ukraine mechi 111 na
kufunga magoli 48 kabla hajastaafu baada ya mashindano ya EURO yaliyofanyika
nchini kwao mwaka 2012, lakini pia akiwa kama nahodha wa timu hiyo, aliweza
kuiongoza timu hiyo katika fainali ya kombe la dunia yam waka 2006.
Shevchenko amesaini mkataba wa miaka miwili
lakini pia akitarajiwa kuongeza mkataba kama atakuwa na mafanikio katika tiku
hiyo. Ukraine itaanza kuisaka tiketi ya kufuzu kombe la dunia la 2018 nyumbani
atakapowakaribisha timu ya taifa ya Iceland mwezi September wakiwa kundi moja
na Uturuki, Croatia, Finland pamoja na Kosovo.
Post a Comment