SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Fainali kugeuka hatua ya mtoano.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
          FAINALI EURO 2012 YARUDISHWA HATUA YA MTOANO Na Charles Kunji Michuano ya EURO2016 inaendelea leo huko nchini ufar...


          FAINALI EURO 2012 YARUDISHWA HATUA YA MTOANO





Na Charles Kunji
Michuano ya EURO2016 inaendelea leo huko nchini ufaransa kwa kuzikutanisha timu ya Italy kuwavaa SPAIN ikiwa ni marudio ya mechi ya fainali ya EURO2012 iliyofanyika huko nchini Poland pamoja na Ukeaine.
Katika fainali hiyo, Italy waliweza kukubali kichapo cha magoli manne kwa nunge na hivyo kuwatawaza mabingwa Hispania wakiwa wamechukua kombe hilo mwaka 2008 lakini pia kuchukua tena kombe la dunia mwaka 2010 lililofanyika kwenye ardhi ya afrika kwa mara ya kwanza.
Katika ushindi wa magoli manne walikuwa ni akina Silva, Alba,Torres pamoja na Mata ndio walioinogesha fainali hiyo huku wakipeleka msiba mzito nchini Italy.
Leo June 27 wanakutana tena katika mashindano hayahaya lakini ikiwa ni hatua ya mtoano. Swali la timu ya Italy kulipiza kisasi litajibiwa baada ya filimbi yamwisho ya mwamuzi wa mchezo huo.
Mechi nyingine ya siku ya leo itawakutanisha England wakiwakabili Iceland huku kukiwa na habari zisizo njema sana kwamba yule mnyama anayetabir mechi mbalimbali, akitabiri ya kuwa England watapoteza mchezo huo. Macho na masikio ya wapenda soka yatakuwa yakisubiri kwa hamu matokeo ya mechi hii.
Lakini katika michezo ya siku ya jana, Wenyeji ufaransa walitokea nyuma na kuweza kushinda mechi yao dhidi ya Ireland ushindi wa magoli mawili kwa moja yote yakiwekwa wavuni na mshambuliaji wa kimataifa Antonio Greezeman anayekipika katika klabu ya Athletical Madrid ya nchini Hispania.
Mabingwa wa kombe la dunia mwaka 2014 waliweza kuwabugiza Slovkia mabao matatu kwa sifuri magoli yaliyowekwa kimwani na Jelome Buateng, Mario Gomez pamoja na Julian Draxler huku Mesuit Ozil akikosa mkwaju wa penaty.
Mechi ya mwisho kwa siku ya jana iliweza kushuhudia ubelgiji wakiibuga kwa ushindi mnono wa magoli manne kwa sifuri magoli yaliyofungwa na Toby Alderweireld, Michy Batshua Yannick Ferreira-Carrasco  pamoja na Eden Hazard.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top