Baada ya LIONEL MESSI, wengine wakafuta.

Na Charles Kunji.
Hii ni siku mbaya kwa soka la Argentina, baada ya kushindwa
kutwaa taji la Copa America kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Chile, uliofanyika
asubuhi ya leo, wachezaji wa Argentina mmoja baada ya mwingine wamekuwa
wakitangaza kustaafu kuichezea timu yao ya taifa.
Mchezaji
wa kwanza kutangaza kustaafu kuitumikia timu hiyo alikuwa Leo Messi ambaye
alitangaza uamuzi huo muda mfupi baada ya mchezo dhidi ya Chile kumalizika.
Maamuzi hayo yaemukuja punde baada ya Lionel Messi kukosa mkwaju
wa penalty uliopelekea timu yake ya taifa kulikosa kombe la Copa Amerika kwa
mara ya pili mfululizo mikononi mwa Argentina.
Muda
mfupi baadaye striker wa Manchester City Sergio Aguero na mlinzi wa kati wa FC
Barcelona Javier Mascherano nao pia walitanga kuachana na timu katika soka la
kimataifa.
Kama
vile haitoshi, ripoti kutoka Amerika ya Kusini zinadai kuwa, Angel Di
Maria, Ezequiel Lavezzi, Gonzalo Higuain na Lucas Biglia nao pia
wameamua kutundika daruga kuitumikia Argentina.
Laikini
kocha wa timu hiyo Tata Martino hajachukua uamuazi wa kuikacha timu hiyo na
labda tumpe muda ni linin aye atatoa hatima yake ama ataendelea kuitumikia timu
hiyo au laaah.
Post a Comment