Na Charles Kunji
Hakika ule msemo usemao, mtu hawezi kufa mara mbili umeweza
kujidhihirisha katika dimba la stade de france baada ya kushuhudiwa mabingwa
watetezi wa kombe la EURO kufungwa 2-0 dhidi ya timu ya taifa ya Italy.
Katika mchezo uliozikutanisha timu hizi kawenye kombe la EURO
2012, katika hatua ya fainali, Italy iliweza kukubali kichapo cha magoli 4-0
magoli yaliyopachikwa kimiyani na Alba, Torres, Silva pamija na Mata na
kuifanya uhispania kunyakua kombe hilo.
Katika mashindano ya EURO2016, Hispania na Italy wameweza
kukutana katika hatua ya 16 bora yaani hatua ya mtoano na kushuhudia timu ya
taifa ya Italy kuibuka na ushindi wa magoli 2-0 magoli yaliyowekwa nyavuni na Girgio
Chiellin pamoja na pamoja na Graziano Pelle mshambuliaji wa kimataifa
anayekipiga katika klabu ya Southampton ya nchini wingereza.
Timu ya taifa ya Hispania iliyosheheni majina makubwa kama
vile David Silva, Busqet, Iniesta, David Degea, Norito pamoja na wengineo
wengi, ilikuwa inapewa nafasi kubwa ya kufanya vizuri n ahata kuchukua kombe
hilo lakini mambo yamekuwa tofauti kwa timu ya Italy kupindua matokeo na kuweza
kufuta uteja kwa uhispania.
Katika mchezo unaoendelea, wingereza bado iko nyuma kwa goli
2-1 dhidi ya timu ya Iceland. Magoli ya Iceland yametiwa kimyani na Ragnar
Sigurdsson na Kolbeinn Sigthorsson huku goli la wingereza likifungwa na nahodha
Wayne Rooney kwa mkwaju wa penalty katika dakika ya 4 ya mchezo.
Post a Comment