MESSI KUSTAAFU TIMU YA TAIFA.

Na Charles Kunji.
Mshambulizi wa Argentina na Barcelona Lionel Messi amestaafu kucheza soka
la kimataifa.
Mchezaji huyo bora
zaidi duniani alitangaza hatua hiyo baada ya kukosa penalti iliyoiwezesha Chile
kuilaza Argentina katika fainali ya michuano ya Copa America.
"Kwangu mimi
,soka ya kimataifa ama hata kuichezea Argentina sitaweza tena.
''Nimefanya kila
niwezalo.''
''Kwa kweli inaniumiza
kuwa sijawahi kutwaa kombe lolote la kimataifa'' alisema mshambulizi huyo
mwenye umri wa mia 29.
Mshambulizi huyo
ameisaidia mabingwa wa ligi kuu ya Uhispania Barcelona, kutwaa mataji 8 na
mataji manne ya ubingwa wa bara ulaya.
Hata hivyo kimataifa
Messi amewahi kushinda taji moja tu lile la nishani ya dhahabu ya Olimipiki ya
mwaka wa 2008 Olympic.
Argentina imeshindwa
katika fainali tatu za kimataifa.
Argentina
walilazwa moja kwa nunge na Ujerumani katika kombe la dunia la mwaka wa 2014
huko Brazil.
Timu
hiyo aidha imeshindwa na Chile mara mbili katika fainali za mchuano wa Copa
America kupitia kwa mikwaju ya penalti.
Messi
vilevile alikuwa katika kikosi kilichoshindwa na Brazil katika mchuano huo wa
mwaka wa 2007 wa Copa America .
Argentina
walitoka sare ya 0-0 baada ya muda wa kawaida na ule wa ziada.
Hata hivyo Chile
waliibuka videdea kwa mabao 4-2 kupitia mikwaju ya penalti.
Messi
alipoteza mkwaju wa kwanza.
Akiwa
Uhispania Messi ametikisa wavu mara 453 kati ya mechi 531 alizoshiriki.
Aidha
Messi ndiye anayeshikilia rekodi ya mfungaji bora wa La Liga akiwa na mabao
312.
Leo anafikia
maamuzi ya kujiuzulu kucheka soka la kimataifa baada ya kuona ameshindwa
kuisaidia timu yake kuchukua kombe lolote historia ambazo ziliwekwa na
wachezaji wa zamani wa Argentina kama vile Diego A lmando Maladona aliyeisaidia
timu yake ya taifa kutwaa kombe la dunia katika mwaka 1986
Kiumri bado
Lionel Messi anaweza kuichezea timu yake ya taifa angalau kwa mwashindano ya
FIFA yajayo yatakayofanyika mwaka 2018.
Amefikia
maamuzi hayo baada ya kuandamwa katika mitandao ya kijamii na yeye pia kujifeel
guilty ni kwa namna gani ameshindwa kuisaidia timu yake ya taifa kuweza kufanya
vyema.
Post a Comment