MAZEMBE HISTOR

NA charles kunji
Ilikuwa
ni mwaka 1939 kitika mji wa elizabethvile ambao kwa sasa ukifahamika kama
Lubumbashi, mmisionari mmoja akifahamika kwa jina la Benedictine aliyekuwa akiiongoza taasisi ya
saint Boniface yaani mtakatifu Boniface alipamua kuanzisha timu ya mpira wa
miguu ikifahamika kwa jina la saint georges, Katika kikundi cha vijana wa skout
kwaajili ya kutoa burudani.
Jina
la la saint georges lilikuwa ni jina la patron wa kikundi cha vijana wa scout.
Tangu
kuanzishwa kwa timu hiyo, mashindano yake ya kwanza saint Georges iliweza kumaliza katika nafasi ya tatu. Nyuma ya fc
leopard ya prince Charles kwa sasa ikifahamika kama VIJANA KATUBA pamoja na
klabu ya Lubumbashi.
Saint georges iliweza
kuvuka katika vipind kadha wa kadha, na katika mwaka 1944 waliweza kubadili jina
na kuitwa saint paul FC baada ya vijana wa scout kuondoka. Miaka kadhaa baadae
baada ya wamisionari kushindwa kuihudumia timu hiyo, ndipo kampuni ya matairi
ikachukua nafasi ya wamisionari na kuibadili timu kwa jina la ENGLEBERT.
Tangu congo ilipopata
uhuru juni 30 ya mwaka 1960 mpaka miaka ya 1966, englebert iliweza kufanyiwa
marekebisho kwa kununua wachezaji wapya
waliokuja kutia chachu klabuni na kuifanya klabu hiyo kuchukua makombe ikiwemo
Katanga cup pamoja na CONGO CUP.
Katika
miaka minne mfululizo iliyocheza englerbert katika fainali ya klabu bingwa
Africa, englebert ilifanikiwa kuchukua mataji mawili kati ya manne iliyocheza
kuanzaia mwaka 1967-70.
Mbali
na AL AHLY YA MISRI ILIYOCHUKUA mara 8 katika ngazi ya vilabu barani Africa,
LITUPISWA ENGLEBERT MAZEMBE wao wamenyanyua kwapa mara tano.
Mafanikio
na changamoto ni mambo yasiyoepukika waliyopitia klabu ya englebert MAZEMBE,
lakini mafanikio ni pale walipoweza kufika katika hatua ya fainali ya clabu
bingwa ya dunia mwaka 2010 iliyofanyika katika mji wa abbuu dhabi huko uarabuni walipoweza kukubali kichapo cha
magoli matatu kwa sifuri toka kwa internationali milan iliyokuwa chini ya
hoseph morinho.
Katika
mashindano ya klabu bingwa barani Africa mwaka 2011 katika hatua ya pili ya mashindano
hayo, mazembe walipangwa kukutana na klabu ya simba ya jijini dar es salaam na
katika mechi zote mbili wekundu wa msimbazi simba wakaweza kulala kwa jumla ya
magoli sita kwa tatu. Baada ya mechi hiyo, milango ya mbwana ally samata ikawa
imefunguliwa na kupata nafasi ya kusajiliwa na klabu hiyo na kuisaidia timu
hiyo kuchukua makombe kadha wa kadha lakini pia kumpelekea samata kuchaguliwa
kuwa mchezaji bora wa mwaka wa wachezaji wa ligi ya Africa.
Siku
ya jumanne ya wiki ijayo, Mazembe watajitupa uwanjani dhidi ya klabu ya kutoka jijini
dar es salaam , wakati huu si wekundu wa msimbazi tena, wala wa matopeni, bali ni wana manjano wa mtaa
wa jangwani hawa ni young African sports clubyaani yanga wa kimataifa. Katika
mchezo wa kundi A wa shirikisho barani Africa.
Sekunde
na dakika vyote vinakimbia kwa speed kuelekea tarehe ishirini na nane ya mwezi
wa sita saa kumi za jioni wakati mwafaka wa mechi hiyo.
Kila
la kheri young African sports club kuelekea mchezo huo, mkiingia kwa tahadhari
ya kuwa mnacheza na clabu kubwa duniani.
Post a Comment