
BAADA ya kusambaa kwa
picha kwenye mitandao ya kijamii ya aliyekuwa kocha wa zamani wa Yanga, Hans
Van Pluijm, juu ya kujiunga na Singida United, sasa ni rasmi kocha huyo atakuwa
mkufunzi wa klabu hiyo.
Pluijm ametia kandarasi
ya miaka miwili na hivyo anatarajia kuleta mapinduzi makubwa kwenye soka la
bongo kwa uzoefu ambao tayari alishakuwa nao.
Uongozi wa Singida United umetoa taarifa rasmi kwa umma
kuthibitisha kumsainisha kocha huyo mkataba wa miaka miwili kuwa kocha mkuu wa
timu hiyo.

Hans alikuwa kama mkurugenzi wa benchi la ufundi la Yanga
ambao waliamua kusitisha mkataba wake baada ya kuona cheo hicho hakikuwa na
maana sana kwa sasa.
Hans ametambulishwa na kinda mwingine Tafadwaza Katinyu
kutoka Zimbabwe kama mchezaji na kuja kuongeza nguvu ya kiungo ya klabu ya
Singida United ambao ni wageni wa ligi kuu ya VPL.
Post a Comment