
HII ni habari njema kwa mashabiki wa
soka nchini Tanzania baada ya nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania, na
mshambuliaji wa klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji Mbwana Ally Samatta kuendelea
kufanya vyema kwenye soka la kulipwa huko barani ulaya.
Muda mchache uliopita Genk walikuwa na mchezo wa marudiano wa
Europa League na kufanikiwa kusonga mbele baada ya kulazimishwa sare na
mahasimu wenzao toka nchini humo klabu ya Gent.
Mchezo wa awali ulimalizika kwa Genk kushinda jumla ya mabao
5-2 huku Samatta akipachika wavuni magoli mawili na baada ya sare ya leo, Genk
sasa wanafuzu hatua ya robo fainali kwa jumla ya mabao 6-3.
Licha ya kucheza dakika zote 90, Samatta hakufanikiwa
kuzifumania nyavu ma hivyo kushindwa kuendeleza moto wake wa kufumga mechi nne
mfululizo.
Samatta anakuwa mchezaji wa kwanza toka Tanzania kufika hatua
ya robo fainali ya michuano ya Ulaya na hivyo kusubiri droo itakayopangwa hapo
baadae.
Hata hivyo Samatta mwenyewe alipokuwa akifanya mahojiano na
mtangazaji wa kipindi cha sports extra cha clouds, bwana Shaffih Dauda, Samatta
alionyesha waziwazi ya kuwa anatamani kupangwa na klabu ya Manchester United
kwani anahisi ndoto zake zitakuwa zimetimia.
Post a Comment