SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: SERENGETI BOYS KWENDA KUJICHIMBIA MADAGASCAR.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Timu ya taifa ya vijana umri chini ya miaka 17 Serengeti Boys inatarajiwa kuondoka alfajiri ya kesho kuelekea nchini Madagasca ku...




Timu ya taifa ya vijana umri chini ya miaka 17 Serengeti Boys inatarajiwa kuondoka alfajiri ya kesho kuelekea nchini Madagasca kuweza kuweka kambi ya kujiandaa na mchezo dhidi ya Africa ya Kusini wa fainali za kombe la mataifa ya Africa chini ya 17 zitakayofanyika mwakani huko nchini Madagascar.

Serengeti Boys imefuzu kucheza na timu ya taifa ya vijana ya Africa Ya Kusini baada ya kuwabugiza magoli 9-0 timu ya taifa ya vijana ya Mauritius na hivyo kusonga mbele na kukutana na timu ya Africa ya Kusini mchezo wa kwanza ukipigwa huko nchini Africa Ya Kusini na kuja kumalizia hapa nyumbani.

Bingwa mtetezi wa mashindano hayo, ni timu ya Mali iliyoifunga timu ya taifa ya Africa ya Kusini kwa jumla ya goli 2-0 katika fainali zilizofanyika nchini Gabon mwaka jana, na mwaka ujayo mwemyeji wa mashindano haya ni Madagasca sehemu ambako Tanzania inakwenda kuweka kambi yake kabla ya kuwavaa timu ya Africa Kusini tarehe 5 ya mwezi agosti kabla ya wao kusafiri kuja jijini Dar es salaam.

Mbali na vijana wa Tanzania kuendelea kuisaka nafasi hiyo kwa udi na uvumba, lakini pia, fainali za mwaka 2019 zitafanyika katika ardhi ya nyumbani kwa hiyo Serengeti boys wakifuzu fainali za mwaka kesho, watakuwa na nafasi nzuri, kwani watakuwa wamepata uzoefu wa kutoka ambapo mashindano yatakuwa katika ardhi ya nyumbani.

Kila la kheri timu yetu ya Tanzania katika maandalizi kuelekea mchezo huyo utakaopigwa tarehe 5 ya mwezi ujao.



About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top