SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: SIMBA SC FANS WAKISHINIKIZA MO APEWE TIMU
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Mashabiki wa klabu ya Wekundu wa Msimbazi Simba wamekusanyika makao makuu ya klabu hiyo maeneo ya Kariakoo mtaa wa Msimbazi wakis...




Mashabiki wa klabu ya Wekundu wa Msimbazi Simba wamekusanyika makao makuu ya klabu hiyo maeneo ya Kariakoo mtaa wa Msimbazi wakishinikiza timu ikabidhiwe kwa MO DEWJI huku viongozi wa klabu hiyo wakiwa hawataki kufanya zoezi hilo.

Hapo jana mfanyabiashara huyo alikuwa na mkutano na waandishi wa habari akitaja vipaumbele vilivyomfanya Dewji kutaka kuinunua klabu hiyo huku swala kubwa likiwa ni kama mshabiki mkereketwa lakini akisisitiza ya kuwa hana maana ya kuinunua klabu hiyo kwa nia ya kumuingizia hela kwani tayari yeye alishakuwa na vyanzo si chini ya 100 ambavyo vinamuingizia kipato chake, hivyo anaitaka hisa ya asilimia 51 ya klabu hiyo.


Uongozi wa klabu hiyo tayari umepanga kuwa na mkutano wa wanachama utakaofanyika hapo kesho ikiwa ni juu ya kutaka kumwachia timu MO na kujadili mambo mengine kadha wa kadha haswa swala la Simba day litakalofanyika siku ya tarehe 8 ya mwezi ujao huku wakuazimisha miaka 80 ya kuanzishwa kwa klabu hiyo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top