
Wakati
timu ya taifa ya Wales ikiwashangaza mashabiki wa mpira wa miguu kwa kufanya
vyema katika mashindano yaanyoendelea nchini Ufaransa, licha ya kutolewa katika
hatua ya nusu fainali dhidi ya timu ya taifa ya Ureno, iliwalazimu Wales
kusubiri hadi miaka 58 ya kuwa na kizazi bora kabisa cha wachezaji waloiinyesha
ubora wa hali ya juu.
Kufuzu
katika michuano mikubwa kama hii, kwa mara ya mwisha taifa hili dogo likiwa
sehemu ya nchi ya Uingereza, ilikuwa ni mwaka 1958 na tangu hapo hawajafanya
vyema mpaka kizazi cha akina Gareth Bale pamoja na Aron Ramsey walioweza
kuiongoza timu ya Wales kufika hapa ilipofika. Pengine unaweza usitambue
umuhimu wa timu ya vijana, Cape Verde lakini unapoona Mataifa kama Cape Verde,
Mouritius wakifanya vyema walikubali kusubiri hadi hapo watakapokuwa na timu
bora ya vijana na kuwakuza ambao sasa wanifanya Cape verde waingie tano bora ya
Mataifa ya Africa katika viwango vya FIFA.
Tanzania
pamoja na kuitwa majina mengi yakiwemo, kichwa cha mwendawazimu sababu ikiwa ni
kutokufanya vyema kwa timu yetu ya Taifa, Taifa stars pamoja na vilabu vya
nchini, ni ile sababu ya kutokuthubutu kuwekeza katika soka la vijana ambao
ndio kizazi cha kesho.
Msingi
wa timu ya taifa hauko kwa akina Nadir Haroub Ally Kanavaro ambao kesho na
keshokutwa wanastaafu kucheza soka kwa sababu ya umri wao kuwa mkubwa. Napatwa
na mshangao kuona Kanavaro anapotangaza kustaafu mpira watu wengi
wakimsikitikia badala ya kumkuza Nickson Kibabage mwenye umri wa miaka 16
kwaajili ya taifa la kesho.
Hatuoni
taabu kujiita tunajenga timu itakayokuja kututoa kimasomaso huku tukimtukuza
John Bocco ambae kesho na keshokutwa anatundika daruga kwa sababu ya umri wake.
Kama
tunataka timu ya kucheza mataifa ya Africa mwaka 2019, hatuna budi kuwakumbatia
vijana wa umri chini ya miaka 17 watakaoweza kuwa na uwezo na kuhakikisha
katika suala la umri, lakini pia vijana hao wakapewa malezi bora na kutafutiwa
mashindano mengi ili kuwatengenezea uzoefu. Timu ya taifa chini ya miaka 17
iliyoenda nchini India kwa mwaliko na kufanya vyema lakini pia kuweza kuwafunga
timu ya vijana ya Misri, ule ndio msingi wa kuanzia.
Lakini
si ajabu timu ya taifa ya Misri ya vijana iliyofungwa na taifa stars katika
mechi ya kirafiki, timu hiyo hiyo ikija baada ya miaka mitano, pengine
ikarudisha kisasi cha kufungwa wakiwa watoto.
Katika
masuala ya mpira hakuna uchawi ni namna nchi wakishirikiana na shirikisho lenye
dhamana ya kusimamia masuala ya mpira ili kuendeleza mashindano kwa vijana kama
itakavyokuwa msimu ujao ambapo timu za vijana za vilabu zitakuwa zinacheza
kabla ya kupisha mechi za wakubwa.
Hii
ndio karata dume, na viongozi wenye dhamana wakisimamia vyema, hakika
mashindano ya matifa ya Africa yam waka 2019 yatakuwa yanatuhusu sana nap
engine hata kufuzu kwa kombe la dunia la mwaka 2022 itakuwa ni halali yetu. Na
ndio maana hata Wales walipotolewa, hawakuwa na sababu ya kusikitika kwani hata
hatua ile, kwao ilikuwa ni mafanikio makubwa sana. Tuwatunze, tuwalinde, kwani
vijana ni taifa la kesho.
Post a Comment