
LIGI kuu nchini England
imerejea tena kwa kasi ambapo leo kwenye mchezo wa awali ulikuwa ukiwakutanisha
mahasimu wa ligi hiyo, klabu ya Liverpool waliokuwa na kibarua cha kuwakabiri
Everton kwenye uwanja wa nyumbani wa Liverpool, Anfield.
Dakika 90 za mtanange huo
zimemalizika kwa Liverpool kuibuka na ushindi wa magoli 3-1 na hivyo kujikita
kwenye nafasi za juu za msimamo wa ligi hiyo mpaka nafasi ya tatu. Kwa jumla ya
pointi 59.
Alikuwa na Sadio Mane
aliyeanzisha hazina ya mabao ya Liverpool mnamo dakika ya 8 akigongea pasi
mujarabu na Roberto Firmino.
Hata hivyo goli la Mane halikudumu kwani dakika ya 28 beki wa Everton,
Matthew Pennington alipachika bao na hivyo kufanya ubao ukisomeka 1-1 na mpaka
dakika 45 zinamalizika, Coutinho akaifungia Liverpool bao la pili na hivyo
kufanya timu hizo kwenda mapumziko kwa liver kuongoza kwa 2-1.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo kila timu ilikuwa inatafuta
nafasi ya kufunga goliili kuibuka na ushindi wa pointi tatu.
Dakika ya 60, Divock
Origi akapachika bao la 3 kwa Liverpool na goli la ushindi kwenye mchezo huo
uliomalizika muda si mrefu.
Kwa matokeo hayo
Liverpooll wanajikita kwenye nafasi ya 3 wakiwa na pointi 59 nyuma ya vinara wa
ligi hiyo klabu ya Chelsea walio na pointi 69.
Post a Comment