SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: LEROY SANE ATUA MAN CITY.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Klabu ya Manchester Vity imekamilisha dili la kumsajili aliyekuwa mchezaji wa klabu ya Shakle kwa kitita cha pauni mil 37. Sane, aliisa...

Klabu ya Manchester Vity imekamilisha dili la kumsajili aliyekuwa mchezaji wa klabu ya Shakle kwa kitita cha pauni mil 37. Sane, aliisaidia Ujerumani kutinga nusu fainali ya mchuano ya Euro 2016, aliifunga klabu yake ya Schalke mabao 33 katika ligi kuu ya Ujerumani. Schalke ilimaliza msimu katika nafasi ya 5.
''Ukimtizama akicheza unavutiwa na ueledi wake, yaani hababaishwi na mpira wala hasuisui hata anapopewa mpira katika mazingira magumu'' alisema Guardiola.
''Hivi unavyomuona ana umri wa miaka 20 tu lakini tayari ameshajishindia nafasi katika timu ya taifa, hiyo inatudhihirishia kuwa anakipaji kinachohitaji kunolewa kisha anawiri kitaaluma''
Kwa upande wake Sane amesema kuwa moja ya sababu kuu yake ya kujiunga na Man City ni kupata nafasi ya kujifua chini ya ukufunzi wake Guardiola.
‘‘Wakati huu katika taaluma yangu hii bila shaka Guardiola ndiye kocha ambaye ninahakika atanifaa zaidi na kunikuza'' alisema Sane. ''Sitarajii kupewa nafasi moja kwa moja ila najua baada ya muda nitapata nafasi''


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top