SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: JORGE COSTA APEWA MKATABA WA MIEZI SITA KUWA KOCHA WA GABON.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
JORGE COSTA amechaguliwa tena kuwa kocha wa timu ya taifa ya Gabon kwa miezi sita. Costa 44, raia wa Ureno, awali alichaguliwa kuwa k...
Jorge Costa



JORGE COSTA amechaguliwa tena kuwa kocha wa timu ya taifa ya Gabon kwa miezi sita.
Costa 44, raia wa Ureno, awali alichaguliwa kuwa kocha mwaka 2014, lakini mkataba wake ulimalizika tarehe 30 ya mwezi juni, na Gabon walishaanza kuandaa kuongeza nae mkataba mwingine.
Costa amekuwa akisuka mipango ya fainali za kombe la mataifa ya Africa ambazo zitafanyika nchini humo mwaka kesho.
‘‘Ni mkataba wa malengo ya wazi na ukiwa kama msingi wa timu yetu ya taifa kuhakikisha inafanya vyema katika ardhi ya nyumbani” Alisema mwenyekiti wa shirikisho la mpira nchini humo.
Lakini pia wakaongeza ya kuwa sababu zingine nje ya uwanja zitawekwa sawa ili kuhakikisha wanampa mwalimu mazingira sawia ya yeye kufanya kazi ili aipe mafanikio timu yao ya taifa.
Costa aliyewahi kuwa beki wa timu ya taifa ya Ureno, amefundisha timu anuwai katika nchi yake lakini pia hata nje ya taifa lake kama vile Cyprus na Romania.
Katika kibarua chake cha awali akiiongoza timu ya taifa ya Gabon, walitolewa katika hatua za awali ya kufuzu kombe la dunia baada ya kushinda mechi moja na kufungwa mechi mbili katika kundi lake.
Mara ya kwanza Gabon kufuzu kombe la dunia ilikuwa ni mwaka 1974 lakini wakashindwa kufuzu tena mpaka mwaka 1994.

Mafanikio yao makubwa ilikuwa ni mwaka 1996 walipofika hatua ya roba fainali na mwaka 2012 walipokuwa wenyeji, wakishirikiana na Equatorial Guiena.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top