
Bilionea Mohammed Dewji ameanza kazi katika klabu ya Simba baada
ya kutoa Sh milioni 100 kusaidia kalbu ya Simba katika masuala ya usajili.usajili.
Mo ametoa fedha hizo leo na kuzikabidhi kwa Rais wa Simba, Evans
Aveva.
Mo alikubali kuisaidia Simba katika usajili wakati mchakato wa kwenda kwenye mabadiliko na kuwa kampuni ukiendelea.
Tayari bilionea huyo kijana ametangaza kuwekeza kiasi cha fedha Sh bilioni 20 ili kupata hisa asilimia 51 ya umiliki wa klabu hiyo na wanachama wameridhia katika mkutano wa wanachama uliofanyika juzi Jumapili.
Mo alikubali kuisaidia Simba katika usajili wakati mchakato wa kwenda kwenye mabadiliko na kuwa kampuni ukiendelea.
Tayari bilionea huyo kijana ametangaza kuwekeza kiasi cha fedha Sh bilioni 20 ili kupata hisa asilimia 51 ya umiliki wa klabu hiyo na wanachama wameridhia katika mkutano wa wanachama uliofanyika juzi Jumapili.
Post a Comment