SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: AFA YAMTANGAZA BAUZA KUWA KOCHA WA ARGENTINA.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Chama cha soka cha Argentina (AFA) kimemteua kocha Edgardo Bauza kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa. Kocha huyu anachukua nafasi iliyoa...
Edgardo Bauza



Chama cha soka cha Argentina (AFA) kimemteua kocha Edgardo Bauza kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa.
Kocha huyu anachukua nafasi iliyoachwa na Gerardo "Tata" Martino aliyejiuzulu baada ya kumalizika kwa michuano ya kombe la Copa America walipokubali kipigo cha mikwaju ya penalty dhidi ya Chile
AFA walimtangaza kocha huyo baada ya klabu ya Sao Paulo kukubali kumuachia kocha huyo kwenda kukinoa kikosi cha timu ya taifa ya Argentina.
Bauza, mwenye umri wa miaka 58, alikua kocha mkuu wa klabu ya Sau Paulo toka mwaka 2015 na kuisaidia kufika nusu fainali ya michuano ya Copa Libertadores, hivyo ataiongoza Argentina katika kampeni za kusaka tiketi ya kombe la dunia la 2018 bila ya staa wa taifa hilo Lionel Messi aliyejiuzulu baada ya kumalizika kwa Copa America.

Makocha waliokua wakipewa nafasi ya kukinoa kikosi hicho ni Jorge Sampaoli Marcelo Bielsa pamoja na Diego Simeon na Mauricio Pochettino.
02 Aug 2016

About Author

Advertisement

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top