Wales wajihakikishia
nafasi ya kusonga mbele.

Na Charles Kunji.
Michuano ya Euro hatua ya robo fainali imendelea tena kwa
mchezo wa pili ambapo timu ya taifa ya Wales imeichabanga vvilivyo timu ya
taifa ya Ubelgiji kwa jumla ya magoli 3-1.
Alikuwa ni Radja Nainggolan dakika ya 13 alipowasimamisha
Mashabiki wa ubelgiji baada ya kuukwamisha mpira wavuni na kuiandikia timu yake
goli la uongozi kabla ya Ashley kurudisha goli dakika ya 31 na kuufanya ubao
usomeke 1-1 mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika.
Kipindi cha pili kilianza kwa mashmabulizi ya kushtukiza kwa
kila timu lakini ilipofika dakika ya 55 Hal Robson-Kanu akaipatia Wales goli la
pili kabla ya Sam Vokes kumalizia mpira kwa kichwa safi dakika ya 86 na mpaka
mwamuzi anapuliza filimbi kumaliza mpira, tayari Wales pamoja na mashabiki wao walikuwa
wamesimama kuishangilia furaha waliyokuwa nayo.

Kwa mara ya mwisho timu ya wales kushinda katika mashindano
makubwa kama haya ilikuwa ni mwaka 1958, na mwaka huu wamefuzu wakiwa chini ya
kocha wao Chris Coleman mpaka wanafika
nusu fainali kucheza na timu ya taifa ya Ureno walioifunga Poland kwa mikwaju
ya penalty 5-4. Baada ya kuushuhudia mchezo wao kwenda dakika 120 wakiwa
wamefungana 1-1
Siri kubwa ya timu ya Wales ni kuwa na mshambuliaji
anayekipiga katika klabu ya Real Madrid Gareth Bale na Aron Ramsey ambao wameweza
kuiongoza timu kucheza kwa umoja na kufika hapa walipofika.
Michuano hiyo itaendelea tena siku ya kesho ambapo timu ya
taifa ya ujerumani itawavaa timu ya taifa ya italia katika hatua ya robo
fainali ya tatu kabla ya mechi ya mwisho katika hatua ya robo fainali ambapo wenyeji
wa michuano hiyo ufaransa watakipiga na timu ya taifa ya Iceland.
Post a Comment