
Na Charles Kunji
Mashindano ya EURO
yameendelea tena usiku, timu ya ureno waliokuwa wanacheza dhidi ya Poland na
kushuhudia Ureno wakifuzu hatua ya nusu fainali baada ya dakika 120 timu zote
kutoshana nguvu ya goli 1-1.
Goli la Poland lilifungwa
na nahodha wao Lewandosk wakati goli la ureno likifungwa na Sanchez.
Wakati mechi inaendelea
kwenye dakika 30 za nyongeza, pasipo kutarajia, katika dakika ya 108 shabiki
mmoja alithubutu kuingia uwanjani kwa ajili ya kumshika Christian Ronaldo
ingawaje maaskari waliokuwako walimdhibi ipasavyo.
Michuano mingine itaendelea
tena kesho wakati timu ya taifa ya Wales watachuana vikali na timu ya taifa ya
ubelgiji wakati robo fainali nyingine itaendelea tena siku ya jumamosi wakati
timu ya taifa ya Italia walio chini ya mwalimu Antonio Conte watakutana na
vijana wa Joachim Low timu ya taifa ya Ujerumani na mechi ya mwisho y6jumapili
wakati wenyeji wa mashindano hayo timu ya taifa ya Ufaransa watawavaa timu ya
taifa ya Iceland kumtafuta atakayeendelea hatua ya nusu fainali ya EURO.
Post a Comment