SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: BALOTELI apewa ruhusa kujiunga na klabu nyingine.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amesema mshambuliaji Mwitaliano Mario Balotelli anafaa kutafuta klabu mpya. Balotelli, 25, ali...




Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amesema mshambuliaji Mwitaliano Mario Balotelli anafaa kutafuta klabu mpya.
Balotelli, 25, alikuwa katika klabu ya AC Milan ya nchini Italy kwa mkopo msimu uliopita lakini amerejea Liverpool kwa mazoezi ya kabla ya msimu.
Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester City amefungia Liverpool mabao manne tangu ajiunge na klabu ya Liverpool msimu wa 2014.

“Hayumo katika kiwango cha uchezaji ambapo anafaa kuwa akishindania nafasi moja au mbili na wachezaji wanne au watano,” amesema Klopp.
“Kwa hivyo, ni wazi kwamba tunahitaji suluhu. Kutakuwa na klabu ambayo itakuwa na furaha kuwa na Mario Balotelli mpya." Alimalizia Klopp.

Baloteli aliyekuwa na msimu mzuri akiwa na klabu ya Manchester City na kufanya vyema, anatarajiwa kujiunga na klabu yeyote itkayaonyesha kumhitaji mwitaliano huyo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top