
Klabu ya Sunderland
imekubali viongozi wa FA kufanya mazungumzo na kocha wao juu ya kuingia mkataba
wa kukinoa kikosi cha taifa ya England.
Lakini klabu ya Sunderland
inayoshiriki ligi ya EPL imesisitiza ya kuwa bado inamhitaji Allardyce kwani
yeye ni mtu muhimu sana klabuni hapo. Allardyce aliweza kuinusuru klabu hiyo
kushuka daraja msimu uliomalizika kwa kumaliza msimu wakiwa wa 17 katika
msimamo mbele ya Aston villa, News castle pamoja na Norwich timu zote zikiwa
zimeshuka daraja.
FA wanahaha kupata saini ya
kocha mwingine baada ya aliyekuwa kocha wa England, Roy Hogson kujiuzulu baada
ya timu yake kutolewa katika hatua ya mtoano [16 bora] na timu ya taifa ya
Iceland kwa magoli 2-1
Sam Allardyce aliye na timu
huko nchini Austria kwa maandalizi ya msimu ujao, anatarajiwa kurudi nchini
Wingereza wiki moja kabla ya kuanza rasmi kwa msimu wa 2016-2017, unaotarajiwa
kuanza rasmi juma la pili la mwezi agosti.
Sunderland wamekubali, japo
kwa shingo upande kwa kujua vyema ile ndio silaha yao, na wamependekeza endapo
kutakuwa hakuna maelewano, basi wasiweze kurefusha mazungumzo.
Post a Comment