SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Mwandishi wa Zamani wa BBC Auawa kwa Kupigwa Risasi.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Aliyewahi kuwa mwandishi wa BBC. auawa Burundi.   ...

Aliyewahi kuwa mwandishi wa BBC. auawa Burundi.

 




Bi Hafsa Mossi, Aliyewahi kuwa mtangazaji wa michezo na habari nyingine katika Shirika la Habari la BBC kupitia Idhaa ya Kiswahili, Hafsa Mossi ameuwawa kwa kupigwa risasi.

Hafsa ambaye alikuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Burundi Hafsa Mossi ameuawa na watu wasiojulikana mjini Bujumbura, leo.

Mtandao wa BBC umesema Hafsa aliyekuwa wakati mmoja Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki katika serikali ya nchi hiyo, aliuawa kwa kupigwa risasi katika barabara ya Gihosha, eneo la Nyankoni.

Msemaji wa rais wa Burundi, Willy Nyamitwe amesema amesikitishwa sana na mauaji ya mwanasiasa huyo.
“Nimesikitishwa sana. Dadangu mkubwa Hafsa Mossi, mwanachama wa @EA_Bunge amefariki, amepigwa risasi na wahalifu. R.I.P #Burundi,” ameandika kwenye Twitter.
Willy Nyamitwea                                   
I'm shocked. My elder Sister Hafsa Mossi Member of the @EA_Bunge has passed away, shot by criminals. R.I.P #Burundi
Waziri wa mambo ya nje Alain Aime Nyamitwe pia ameeleza kusikitishwa kwake na mauaji hayo.
“Nimehuzunishwa sana na mauaji ya leo#Bujumburaya Mheshimiwa Hafsa Mossi, na mwanachama wa#EALA. Ni hasara kuu kwa taifa na#EAC,” ameandika kwenye Twitter.



About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top