SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: SIMBA KATIKA UBORA WAO.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Klabu ya wekundu wa Msimbazi Simba, wameendelea na michezo ya kirafiki huko mjini Morogoro, ambapo jana tena walikuwa uwanjani na k...



Klabu ya wekundu wa Msimbazi Simba, wameendelea na michezo ya kirafiki huko mjini Morogoro, ambapo jana tena walikuwa uwanjani na kuwashuhudia wakitoka kifua mbele baada ya kuwafunga klabu ya Burkinafaso kwa ushindi mujarabu wa magoli 5-0

Magoli ya Simba yaliwekwa kimyani na mshambuluaji wao machachari Ibrahimu Ajibu aliyepachika magoli mawili wakati Ndusha akifunga goli moja, na Shiza Kichuya aliyesajiliwa kutoka Mtibwa Sugar naye akafungua hazina ya magoli wakati lile la mwisho likipachikwa nyavuni na Said Ndemla.


Tangu wameweka kambi jijini Morogoro, klabu ya Simba imekwisha cheza mechi 3 akiwa ameshinda zote wakati ile ya awali ilikuwa ni dhidi ya Polisi Morogoro walipowabugiza magoli 6-0 wakati mchezo mwingine ulikuwa dhidi ya Moro Kids waliposhinda goli 2-0 na wakitarajiwa kucheza mchezo mwingine dhidi ya timu ya Manispaa ya Kinondoni na ndipo watarudi jijini Dar kwaajili ya kujiandaa na Simba Day watakapokuwa na mchezo wa kirafiki dhidi ya klabu ya kutoka Angola Inter-crop.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top