SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: DAVID DE GEA; ‘‘UJIO WA IBRAHIMOVIC, UMEONGEZA HAMASA”
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Kipa nambari moja wa klabu ya Manchester United David De gea amesema ujio wa nyota wa Sweden Zlatan Ibrahimovic imeongeza hamasa ya h...
David De Gea is pleased with Manchester United's summer transfer business


Kipa nambari moja wa klabu ya Manchester United David De gea amesema ujio wa nyota wa Sweden Zlatan Ibrahimovic imeongeza hamasa ya hali ya juu kikosini hapo.

Ibrahimovic 34, alipewa jezi yenye namba 9 mgongoni alipofika baada ya kukamilisha dili la usajili huru toka klabu ya PSG ya nchini Ufaransa kuja kuungana na aliyewahi kuwa kocha wake wa zamani Jose Morinho.

Morinho pia amewanunua, beki wa Ivory Coast Eric Bailly na raia wa Armenia  Henrikh Mkhitaryan na De Gea amekubali uwezo wa wachezaji wote kwa muda mchache ambao wamekuwa kwenye mazoezi pamoja.

‘‘Ni jambo zuri sana kuwa na Zlatana hapa tayari, akifanya mazoezi na timu, unaweza kuona ni mchezaji mzuri, akiwa shupavu na sifa zote za kuwa mshambuliaji tayari anazo” De Gea aliiambia MUTV.

‘‘Nafikiri ataendana na mazingira kwa haraka Zaidi, unaweza kuona na anaoneka kama alikuwa anacheza hapa kwa muda mrefu sasa na sawa kwa wachezaji wengine ambao wote tumejumuika nao” Alisema De Gea.

‘‘Wanacheza vizuri sana mazoezi yao yamekuwa ni ya hali ya juu sana na naweza kusema ya kuwa tumesajili watu sahihi ambao wanatupa nguvu, unapoona wachezaji kama wao wanakuja hapa Manchester na sasa tumewajaribu wote kwa pamoja, kujaribu kuwaweka sawa kwa upesi zaidi na sasa tunakwenda kucheza mechi kubwa mechi ya ngao ya hisani dhidi ya mabingwa Leicester city”



About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top