SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: MONTOYA AMALIZANA BA BARCA NA KUJIUNGA NA VALENCIA
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Beki wa kati wa klabu ya Barcelona, Martin Montoya, amejiunga na klabu ya Valencia kwa dili la miaka minne baada ya kuruhusiwa na klab...





Beki wa kati wa klabu ya Barcelona, Martin Montoya, amejiunga na klabu ya Valencia kwa dili la miaka minne baada ya kuruhusiwa na klabu yake huku vilabu vyote vikiwa vimekubaliana kwa pamoja hapo jana.

Montoya 25, raia wa Hispania alipandishwa katika timu ya wakubwa mwka 2011 lakini akashindwa kuonyesha uwezo wake katika mechi zote 45 alizocheza na hivyo kusababisha maisha yake Camp Nou kuendelea kuwa magumu.

Klabu ya Valencia na Montoya mwenyewe wamekwishafikia makubalianoo na hivyo Montoya atasaini kandarasi ya miaka minne kuihudumu klabu hiyo ya Valencia inayoshiriki ligi kuu ya Hispania.


Montoya ametumia muda wake mwingi akiwa klabu ya Inter kwa mkopo pamoja na Real Betis msimu uliopita na anatarajiwa kukiimarisha kikosi cha Valencia akiwa kama sehemu ya kikosi hicho.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top