SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: SHAMRASHAMRA ZA USAJILI BARANI ULAYA.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Klabu ya Southampton imemsajili golikipa Alex McCarthy kwa mkataba wa miaka mitatu toka timu ya Crystal Palace. McCarthy, alicheza michez...
Alex McCarthy
Klabu ya Southampton imemsajili golikipa Alex McCarthy kwa mkataba wa miaka mitatu toka timu ya Crystal Palace. McCarthy, alicheza michezo saba msimu uliopita akiwa na klabu yake ya Crystal Palace huu ni usajili wa tatu wa klabu hiyo ya Southampton baada ya kuwasajili Nathan Redmond Pierre-Emile Hojbjerg.
Steven Taylor
Wakati huo, beki Steven Taylor amejiunga na timu ya Portland Timbers, inayoshiriki ligi ya kuu ya Marekani akitokea Newcastle United. Beki huyo amekaa kwenye klabu ya Newcastle kwa muda wa 21 toka akiwa mdogo, na amecheza michezo 268.
Alex Song
Na timu ya Rubin Kazan imemsajili kiungo Alex Song bure kwa mkataba wa miaka mitatu kutoka kwa miamba wa Hispania Barcelona. Song aliitumika West Ham msimu uliopita kwa mkopo baada ya kukosa nafasi ya kudumu katika kikosi cha Barcelona.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top