SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: MARLOS MORENO ASAJILIWA MANCHESTER CITY.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Na mwandishi wetu, Charles Kombe. Matajiri wa jiji la Manchester, Klabu ya Manchester City wamemsajili mchezaji kut...



Na mwandishi wetu, Charles Kombe.

Matajiri wa jiji la Manchester, Klabu ya Manchester City wamemsajili mchezaji kutoka Colombia, Marlos Moreno kwa kitita cha paun milioni 4.75 kwa kandarasi ya miaka mitano.

Kinda huyo mwenye umri wa miaka 19 atakwenda klabu ya Uhispania Deportivo La Coruna kwa mkopo msimu wa 2016/17.

Marlos Moreno anakuwa mchezaji wa tatu kusainiwa na Pep Guardiola katika wiki hii, baada ya kuwasili kwa winga Leroy Sane kutoka clab ya Schalke 04 pamoja na kinda wa Brazil Gabriel Jesus Kutoka klabu ya Palmeiras ya nchini Brazil.

Tangu Mhispania huyo achukue nafasi ya Manuel Pellegrini kama meneja mwezi julai, Guardiola ametumia kiasi cha £100m hadi kufikia sasa.

Moreno aliandika katika wavuti ya clab hiyo kuwa “ "Pep Guardiola ni moja ya mameneja bora duniani. Nadhani anapenda wachezaji chipukizi zaidi na anaweza kuwafunza zaidi wachezaji chipukizi kwa mbinu pamoja na ufundi, Itakuwa jambo kubwa sana kufanya kazi naye na kua miongoni mwa timu kubwa” alisema Moreno.

Hata hivyo katika kuimarisha kikosi chake, Bosi huyo wa zamani wa Bayern Munich na Barcelona Pep Guardiola amelipa kipaumbele swala la kuwasajili wachezaji chipukizi watakao kuwa ghali zaidi katika kipindi kijacho.

Muispania huyo pia ana ndoto za kumsajili beki wa Everton na timu ya taifa ya England Johns, ambapo clab hiyo ya England imetangaza kutaka paun mil.50 kwa timu itakayomsajili beki huyo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top