
Katika mwendelezo wa mechi za kirafiki zinazoendelea, mchezo kati
ya klabu ya Liverpool na Barcelona umeweza kumalizika kwa Klabu ya Barcelona kukubali
kufungwa goli 4-0 dhidi ya klabu ya Liverpool iliyo chini ya mwlimu Jugen
Klopp, raia wa Ujerumani.

Ushindi mujarabu wa Liverpool ulifunguliwa dakika ya 15,
ambapo mchezaji ingizo jipya aliyesajiliwa toka klabu ya Southampton Sadio Mane
alipoukwamisha mpira wavuni, kabla ya Mascherano kujifunga wakati Divock Orig
na Grucij wakikamilisha idadi hiyo ya magoli manne.
Mabingwa hao wa ligi ya Hispania, klabu ya Barcelona
walipanga kikosi chote isipokuwa yule mchezaji wao muhimu Neymer ambae
analitumikia taifa lake katika mashindano ya Olympic yanayoendelea huko Rio
nchini Brazil.

Klopp amesema japo wameshinda, lakini bado hawako vizuri sana
nab ado ana kazi ya kukitengeneza kikosi hicho ili kiwe kikosi cha ushindani na
hadhi ya klabu hiyo iweze kurejea kama zamani.
Post a Comment