SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: KAULI YA NAPE JUU YA TIKETI ZA KIELEKTRONIC.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
picha na salehe jembe. WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, amesema tayari wameshakamilisha mfumo wa utum...




picha na salehe jembe.


WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, amesema tayari wameshakamilisha mfumo wa utumiaji wa tiketi za elektroniki kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, na muda wowote zitaanza kutumika.

Ni kwa muda mrefu serikali ilitangaza kuweka mfumo wa tiketi hizo kwenye viwanja inavyovimiliki vya Uhuru na Taifa, lakini suala hilo lilionekana kama kusuasua kabla ya hivi karibuni kutiliwa mkazo na hatimaye kukamilika.

Awali ilielezwa kuwa, Jumapili iliyopita ndiyo serikali itakabidhiwa mfumo huo baada ya kukamilika, lakini zoezi hilo likaahirishwa kutokana na shughuli za kiserikali kuingiliana.

“Kila kitu kimekamilika na nimehakikishiwa hilo na wale tuliowapa kazi hiyo, ile ratiba ya awali ya kukabidhiana nimeiahirisha mimi na si mwingine kwa sababu siku tuliyopanga awali mimi nilikuwa Dodoma kwenye shughuli nyingine za kiserikali.” Nape alisema.

Nape alisisitiza kuwa, wikiendi hii ndiyo wanatarajia kulifanya zoezi hilo la makabidhiano.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top