
SHIRIKISHO la mpira wa miguu nchini TFF,
limeanda semina elekezi kwa klabu za Ligi Kuu za wanawake ikiwa ni sehemu ya
maandalizi ya ligi hiyo inayotarajia kuanza rasmi mapema mwezi ujao.
Semina
hiyo iliyokuwa ifanyike siku ya jumamosi, inaendelea sasa hivi kwenye Ukumbi wa
Hosteli za TFF zilizopo ofisi za Makao Makuu ya shirikisho hilo Uwanja wa
Kumbukumbu ya Karume ulioko makutano ya barabara za Shaurimoyo na Uhuru jijini
Dar es Salaam.
Ligi hiyo
ya wanawake ni ya kwanza kufanyika nchini chini ya uongozi wa Rais Jamal
Malinzi kwani kabla ya hapo hapakuwa na ligi inayohusisha mikoa mbalimbali.
Shukrani za pekee ziende kwa Kituo cha Televisheni cha Azam, kilichoamua
kudhamini ligi hiyo pamoja na ile ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 20.
TFF
imeandaa semina hiyo kwa ajili ya kuwapa maelekezo kuhusu kanuni za ligi,
usajili wa timu na taratibu nyingine za ligi hiyo ikiwa ni pamoja na sheria za
mpira wa miguu ambazo zimekuwa na marekebisho kwa msimu wa 2016/2017 kama
zilivyotolewa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).
Post a Comment